2020-04-11 07:38
8144 243
Waziri Mkuu Majaliwa amekutana na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke na ameishukuru China kwa misaada ambayo imetoa katika kukabiliana na corona>> “ugonjwa China umepungua, tunawashukuru pia kwa kukaa na Watanzania wetu kule,mmewahudumia Wanafunzi wetu” •
•
“Tunaishukuru Serikali ya China kwa misaada ambayo imetupatia hadi sasa vikiwemo dawa na vifaa tiba, na leo umesema kuna asasi za kiraia na wafanyabiashara bado wanakusanya vifaa vingine ili viletwe hapa nchini vitusadie kuzuia maambukizi, tunawashukuru sana”-MAJALIWA •
•
Waziri Mkuu ametoa shukrani hizo ofisini kwake Mlimwa, Dodoma alipokutana na Balozi huyo>> “mchango wenu ni muhimu sana kwetu, kwa sababu tunaanza kupata uzoefu wa namna ya kupambana na ugonjwa huu” •
•
Majaliwa amesema Tanzania Bara na Zanzibar zinapata wagonjwa kwa sababu ni vituo vya biashara lakini wageni wote wanaoingia nchini kwa sasa wanawekwa sehemu maalumu ambako wanapatiwa huduma zote wakiwa hukohuko.